watu 10 wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro baada ya kukamatwa
msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi na bendera nyeusi
inayodaiwa kutumiwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab wa nchini
Somalia.Katika tukio hilo, mmoja anayesadikiwa kuhusiana na watu
hao waliokamatwa aliuawa na wananchi wenye hasira baada ya kumjeruhi kwa
panga askari polisi aliyekuwa akipambana naye.
Akizungumza na
waandishi wa habari leo, Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Leonald Paul
alisema tukio hilo limetokea jana (Aprili 14) majira ya saa 3.30 usiku
katika kitongoji cha Nyandero, tarafa ya Kidatu wilayani
Kilombero.Kamanda Paul alimtaja mtu aliyefariki kuwa ni Hamad Makwendo
ambaye umri wake haujafahamika ambaye ni mkazi Manyasini Ruaha wilayani
Kilombero.
Aidha alisema siku ya tukio polisi walipata taarifa
kutoka kwa raia wema kuhusu watu hao na kwamba walitaarifiwa kuwa
wanajihusisha na matukio mbalimbali ya uhalifu na polisi waliamua
kufatilia nyendo zao.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Blogger Comment
Facebook Comment