Wema Sepetu ni mwigizaji staa wa Tanzania hakuna asiejua, Wema Sepetu ni Miss Tanzania 2006 na ni miongoni mwa mastaa wenye ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii, hakuna asiejua…… ila tatizo linalomsumbua kwa sasa inawezekana kuna wengi wasiolijua.
Amekua akisumbuliwa na tatizo la kutoweza kushika ujauzito ambapo baada ya ukimya mwingi, Wema ameamua kuongea yafuatayo kwa wote wanaombeza kutokana na tatizo lenyewe.
Amesema >>> ‘Ningekuwa na uwezo wa kuzaa ningekuwa nimezaa muda mrefu sana… But sina… Na siwezi kumkufuru mwenyezi mungu…. Au mngependa niwe nawaambia jinsi ninavyo hangaika usiku na mchana kupata mtoto wangu mwenyewe… Is dat wat u want…? kila ntakachofanya kwa ajili ya tumbo langu basi nitangaze… Au mnadhani siumii mnavyosema kuhusu maswala ya mtoto‘

‘Kwani kuna niliemkosea yoyote mpaka muanze tu kunikashif na kunitolea maneno mazito namna hio… Kisa mtoto… mnadhani naipenda hii hali… hata mimi natamani kuitwa mama na hakuna kinachoniuma kama hicho…. So mnadhani sijui kama umri unaenda na maisha yenyewe sikuhizi mafupi anytime we die… Mnafikiria nisingependa kuacha hata ka copy kangu siku ndo Mungu anasema ananichukua’
Blogger Comment
Facebook Comment